JINSI YA KUONGEZA UZITO AU UNENE BILA KUDHURU MWILI WAKO

Mon media
0

 



basi ni mhimu kwamba unafanya jambo hili kwa njia salama ambazo hazitakuletea madhara baadaye.


Kunywa soda, kula maandazi au chipsi za vibandani ni vitu vinaweza kukuongezea uzito na unene kwa haraka lakini wakati huo huo vinaweza kuharibu afya yako.


Kama uzito wako upo chini ni mhimu kuzingatia umhimu wa kuongeza uzito sambamba na misuli na siyo kuongezeka uzito pamoja na tumbo au kitambi.


Wapo watu wengi tu wenye uzito sawa na bado wanaugua kisukari aina ya pili, ugonjwa wa moyo na matatizo mengine ya kiafya yanayohusiana na uzito kuwa juu.


Hivyo ni mhimu kwamba bado unaendelea kula vyakula vyenye afya na kuishi maisha yenye afya kila siku.


Tuangalie sasa njia za kuongeza uzito na unene kwa haraka bila kuharibu afya yako:


1. KULA ZAIDI

Jambo la mhimu unaloweza kulifanya ili kuongeza uzito ni kula zaidi ya unavyohitaji mwili wako. Bila hivi ni vigumu kuongezeka uzito.


Kama ulikuwa unakula mara 2 au 3 kwa siku sasa anza kula mpaka mara 5 kwa siku. Muda wote tumbo liwe limejaa. Siyo kiasi cha kuwa kero lakini kuwa makini.


2. KULA ZAIDI VYAKULA VYENYE PROTINI

Lishe moja mhimu zaidi katika kuongeza uzito ni ile yenye protini kwa wingi ndani yake.


Mishipa inatengenezwa na protini na bila kuwa na protini ya kutosha sehemu kubwa ya nishati ya mwili huishia kuwa mafuta.


Tafiti zinaonyesha kuwa wakati unaongeza kiasi cha chakula unachokula, lishe yenye protini nyingi kile kiasi kinachozidi huweza kubadilishwa na kuwa misuli ya mwili.


Hata hivyo elewa hili tena, chakula chohcote chenye protini nyingi huwa na uwezo wa kukupunguzia njaa au hamu ya kutaka kula chakula.


Hili linaweza kukuletea shida tena kuendelea kula zaidi kama moja ya mahitaji mhimu ili kuongeza uzito na unene kwa ujumla.


Hivyo wakati ukiendelea na lishe yenye protini ni mhimu pia kuongeza mbinu za kuongeza njaa ili uendelee kula zaidi.


Vyakula vyenye protini kwa wingi vinajumuisha nyama, mayai (mayai ya kienyeji) maziwa freshi, karanga, mbegu za maboga (kama unahitaji mbegu za maboga zilizokaangwa tayari kwa matumizi niachie ujumbe WhatsApp +255769142586), samaki, korosho nk.


Hivyo protini ni mhimu ili kutengeneza misuli na mishipa kwa ujumla, kula protini ya kutosha ni mhimu ili kuongezeka uzito unaobaki kama misuli na siyo mafuta.


3. KULA ZAIDI WANGA NA MAFUTA

Kula kwa wingi vyakula vyenye wanga na mafuta kama shida yako ni kuongezeka uzito na unene. Ni vizuri katika mlo ule vya kutosha vyakula vyenye wanga, mafuta na protini kwa matokeo mazuri zaidi.


Vyakula vyenye wanga kwa wingi ni pamoja na viazi vitamu, ugali wa dona, wali, mkate, chapati, maandazi, tambi (pasta), maembe, viazi mviringo (chipsi), ndizi, tende, pizza, nk.


Mafuta mazuri yanapatikana katika parachichi na mafuta yake, mafuta ya zeituni, siagi ya karanga, mayai, mafuta ya samaki, mafuta ya nazi, mafuta ya mawese, ufuta na mafuta yake nk.


Hakikisha unakula mara 3 mpaka 5 kila siku mlo wa aina hii.


4. KULA VYAKULA VYENYE NGUVU ZAIDI

Ni mhimu tena kula vyakula vya asili zaidi na vyenye nguvu zaidi. Kama ni ugali kula ugali wa dona na si sembe, kama ni mkate kula mkate wa unga wa ngano ambayo haijakobolewa.


Kwa kifupi tu usile vyakula vilivyokobolewa au vya madukani kama unataka kuongezeka uzito na unene kwa njia salama kwa afya yako.


Pia ongeza viungo zaidi kwenye hivyo vyakula ili kuongeza hamu ya kutaka kula zaidi. Ongeza iliki au mdalasini na viungo vingine vitakavyokufanya upende kula zaidi hicho chakula.


Kula zaidi vyakula hivi kwa kupata nguvu zaidi; lozi, jozi, korosho, karanga, tende, zabibu kavu, maziwa freshi, mtindi, mafuta ya zeituni, parachichi, nyama ya kuku wa kienyeji, nyama ya ng’ombe, nyama ya nguruwe, nyama ya mbuzi, viazi, viazi vitamu, siagi ya karanga nk.


Vingi ya hivi vyakula vina kawaida ya kukupotezea njaa na hamu ya kula hivyo itakulazimu wakati mwingine kujilazimisha tu ili ule zaidi kwa siku.


Pia siyo wazo zuri kula sana mboga za majani kama shida yako ni kuongeza uzito hii ni kwa sababu zitaziba nafasi inayohitajika kukaliwa na vyakula hivi vyenye nguvu zaidi. Pia matunda iwe kidogo labda tunda moja tu hasa parachichi au ndizi moja tu basi.


5. NYANYUA VITU VIZITO

Ili kujihakikishia kuwa hicho kiasi cha chakula ulichoongeza kula kinakwenda kwenye misuli na si kukuletea mafuta na pengine tumbo au kitambi ni mhimu ufanye mazoezi ya kunyanyua vitu vizito.


Nenda gym na unyanyuwe vyuma mara 3 mpaka 4 kwa wiki, anza na uzit

o mdogo na uongeze uzito kidogo kidogo kadri unavyoendelea.

Tags

Post a Comment

0Comments
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top