KOCHA GAMOND YANGA ATANGAZA KUFUTA MACHOZI KWA MAMELOD

Mon media
0


 Kocha wa Young Africans, Miguel Angel Gamondi amesema alidhani atakuwa na mtihani mgumu kuwajenga kisaikolojia wachezaji wake baada ya kichapo dhidi ya Azam FC, lakini amekutana na kitu tofauti kutokana na kikosi chake kuwa morali nzuri na kipo tayari kwa kupambana dhidi ya Mamelodi Sundowns.


“Mpira ni mchezo wa makosa, nyota wangu walikosea kidogo na wakaadhibiwa, wameahidi kupambana kwa kurudisha furaha kwa mashabiki wetu, kitu ambacho nimekifurahia na naamini kitaongeza chachu ya ushindani katika mechi yetu ya Ligi ya Mabingwa Afrika,”


Gamondi amesema baada ya kuona wachezaji wake wamekubali kupoteza na kukubali kuendeleza mapamnbano tayari kwa mchezo unaofuata, amekaa nao na kuwapa namna ambavyo wanatakiwa kufanya kuweza kuanza vizuri mchezo wao wa Jumamosi (Machi 30).


“Huwa napenda kila mchezaji katika kikosi changu kuwa tayari, kwani muda wowote anaweza kutumika kulingana na mahitaji ya mchezo, kila mchezaji kwangu ana nafasi na ndio maana huwa tunawaandaa mazoezini, anayeonakana kufanya vizuri katika mpango wangu hupewa nafasi,” amesema. 

Tags

Post a Comment

0Comments
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top