JAPAN YAANZISHA DATING APP

Mon media
0



Kiwango cha uzazi nchini Japan ambacho kimezidi kushuka kwa kasi kwa miaka mingi na kufikia rekodi nyingine ya chini zaidi hivi karibuni, kimeifanya Serikali ya Nchi hiyo kuongeza ubunifu kwenye kampeni zake za kuwahimiza Vijana kuoa na kuanzisha familia ambapo sasa imezindua APP ya simu ambayo kazi yake mahususi ni kurahisisha Watu kuchumbiana.
 
Kwenye APP hiyo na tovuti yake, Watumiaji lazima wawe ‘single’ wakiwa na umri zaidi ya miaka 18 na wawe wenye hamu ya kuoa na kuolewa pia wawe wanaishi au kufanya kazi katika Jiji la Tokyo ambapo Watumiaji wataombwa kuweka sifa ambazo wanatamani kuzikuta kwa wenza wao wa maisha. 

Ndani ya APP hiyo yenye mambo mbalimbali, pia inaorodhesha hatua nyingine za Serikali kusaidia Wanandoa kama vile kutoa taarifa kuhusu ku-balance kazi na maisha ya ndoa, malezi ya Watoto, kutoa msaada wa Makazi, kuwafundisha Wanaume jinsi ya kushiriki kwenye kazi na majukumu ya nyumbani, kulea Watoto na kutoa ushauri wa ajira na kazi.

Ukiachia mbali viwango vya kuzaliana kushuka Nchini Japan, pia viwango vya Wanandoa kupeana talaka vimeongezeka na kuongeza wasiwasi kwa Serikali ya Nchi hiyo.

Majaribio ya APP hiyo yamevutia wengi akiwemo Tajiri wa dunia Mmiliki wa mtandao wa X pamoja na magari ya umeme ya Tesla Elon Musk ambaye aliandika yafuatayo kwenye X “Nina furaha Serikali ya Japan inatambua umuhimu wa jambo hili, endapo hatua kali hazitochukuliwa, Japan pamoja na Nchi nyingine nyingi zitatoweka” 

 

Tags

Post a Comment

0Comments
Post a Comment (0)

#buttons=(Accept !) #days=(20)

Our website uses cookies to enhance your experience. Learn More
Accept !
To Top